Nafasi ya Kazi Diamond Trust Bank (DTB) Tanzania
Benki ya Diamond Trust Bank Tanzania Plc (DTBT) imetangaza nafasi ya kazi ya Assistant Manager - Debt Recovery kwa mwaka 2026. Hii ni fursa nzuri kwa wataalamu wa masuala ya kibenki, sheria, na fedha kujiunga na moja ya benki kongwe na imara nchini Tanzania.
Kuhusu Diamond Trust Bank (DTB)
Diamond Trust Bank Tanzania ina historia ndefu iliyoanza mwaka 1945 kama Diamond Jubilee Investment Trust (DJIT) kufuatia maadhimisho ya miaka 60 ya uongozi wa Agakhan III. Mnamo mwaka 1965, kampuni hiyo iligawanywa katika matawi ya Tanzania, Kenya, na Uganda. Leo hii, DTB ni mdau muhimu katika uchumi wa Afrika Mashariki, ikitoa huduma bora za kibenki kwa wateja wa kampuni (Corporate) na wadogo (SMEs).
Maelezo ya Kazi: Assistant Manager - Debt Recovery
Msimamizi huyu atakuwa na jukumu la kusimamia urejeshaji wa madeni sugu (NPLs) na mikopo iliyofutwa (Written-Off Facilities). Kazi hii inahitaji uzingatiaji wa sera za ndani ya benki, miongozo ya kisheria, na kanuni za usimamizi wa mikopo.
Majukumu ya Kazi
- Kutathmini hali ya akaunti za wadaiwa na kupendekeza njia bora ya kurejesha fedha za benki kwa haraka.
- Kufanya mazungumzo na wateja wa Corporate, SMEs, na Retail walioshindwa kulipa mikopo ili kufikia makubaliano ya malipo.
- Kusimamia kampuni za kukusanya madeni (Debt Collectors) na madalali wa minada (Auctioneers) ili kuhakikisha wanafanya kazi kwa ufanisi.
- Liaising na idara ya sheria kuhusu mikakati ya kurejesha madeni kwa kesi zilizopo mahakamani.
- Kuhudhuria vikao vya mahakama na usimamizi wa uuzaji wa mali zilizowekwa dhamana kupitia minada ya hadhara au zabuni.
Sifa na Vigezo vya Mwombaji
Ili uweze kufikiriwa katika nafasi hii, unapaswa kuwa na sifa zifuatazo:
- Elimu: Shahada ya Kwanza (Bachelor's Degree) katika Business Administration, Usimamizi wa Benki, Fedha (Finance), Uhasibu, Uchumi, Sheria, au fani inayofanana na hizo.
- Sifa za Ziada: Cheti cha Loan Work-Out, Debt Recoveries, au Credit Risk Management itakuwa sifa ya ziada.
- Ujuzi: Uwezo mkubwa wa kuwasiliana (kwa maandishi na mazungumzo), ujuzi wa majadiliano (negotiation skills), na motisha binafsi.
Jinsi ya Kutuma Maombi
Ikiwa unakidhi vigezo vilivyotajwa hapo juu, tuma barua yako ya maombi pamoja na wasifu wako (CV) kupitia barua pepe ifuatayo:
Barua Pepe: recruitment2026@diamondtrust.co.tz
Mwisho wa Kutuma Maombi: Tarehe 30 Januari, 2026.
Zingatia: DTB Bank ni mwajiri anayezingatia usawa. Maombi yote yatafanyiwa kazi kwa siri kubwa.
